INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Kubwa alilozungumzia ni Bunge la Katiba linaloanza tena wiki ijayo.Ni ndefu sana naangalia namna ya kuwaletea kwa muhtasari au kuleta yote kama ilivyo
HINTS ZA HOTUBA
- Bunge la katiba linajadili RASIMU YA TUME na sio vinginevyo. Wanaosema Bunge halijadili rasimu ya Tume ya Warioba ni Wazushi.
- Sheria inaeleza kuwa Tume inapaswa kuandaa RASIMU ya KATIBA na Bunge la katiba linapaswa kuandika KATIBA INAYOPENDEKEZWA. Kwahiyo Bunge linafanya kazi yake kikamilifu.
- Huwezi kutunga Katiba inayopendekezwa bila kufanya Mabadiliko. Bunge la Katiba lazima lifanye mabadiliko na linaruhusiwa kisheria ili kutekeleza jukumu lake la kutunga katiba inayopendekezwa.
- UKAWA hawana sababu ya msingi ya kutoka au kususia Bunge
- Bunge litaendelea na theluthi mbili ndio itaamua hatma ya Katiba inayopendekezwa na kisha wananchi wataamua kupitia kura ya maoni
Utangulizi
Ndugu wananchi;
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujalia uzima na kutuwezesha kwa mara nyingine tena kuzungumza na taifa juu ya masuala muhimu yanayohusu nchi yetu. Mwezi wa Saba tunaoumaliza leo ulikuwa na matukio mengi baadhi yakiwa makubwa na kushtusha na mengine yalikuwa matukio ya kawaida.
Mashambulio ya Mabomu
Ndugu Wananchi;
Tarehe 3 Julai, 2014 na tarehe 07 Julai, 2014 kulitokea mashambulizi ya mabomu nyumbani kwa Sheikh Sudi Ally Sudi na katika mgahawa wa Vama kwa mfuatano huo. Kabla ya hapo, kulikuwa na matukio mengine matatu: Kanisa la Olasiti tarehe 5 Mei, 2012, Mkutano wa Kampeni wa CHADEMA tarehe 15 Juni, 2013 na Baa ya Arusha Night Park tarehe 13 Aprili, 2014. Hali kadhalika, tarehe 13 Juni, 2014 kulitokea shambulizi la mabomu katika eneo la Darajani, Zanzibar.
Ndugu wananchi;
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujalia uzima na kutuwezesha kwa mara nyingine tena kuzungumza na taifa juu ya masuala muhimu yanayohusu nchi yetu. Mwezi wa Saba tunaoumaliza leo ulikuwa na matukio mengi baadhi yakiwa makubwa na kushtusha na mengine yalikuwa matukio ya kawaida.
Mashambulio ya Mabomu
Ndugu Wananchi;
Tarehe 3 Julai, 2014 na tarehe 07 Julai, 2014 kulitokea mashambulizi ya mabomu nyumbani kwa Sheikh Sudi Ally Sudi na katika mgahawa wa Vama kwa mfuatano huo. Kabla ya hapo, kulikuwa na matukio mengine matatu: Kanisa la Olasiti tarehe 5 Mei, 2012, Mkutano wa Kampeni wa CHADEMA tarehe 15 Juni, 2013 na Baa ya Arusha Night Park tarehe 13 Aprili, 2014. Hali kadhalika, tarehe 13 Juni, 2014 kulitokea shambulizi la mabomu katika eneo la Darajani, Zanzibar.